Close Menu
KahawaTunguKahawaTungu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawaTunguKahawaTungu
    Subscribe
    • HOME
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
      • AFCON
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    • OBITUARIES
    • JOBS
    KahawaTunguKahawaTungu
    Home » Wasichana Waliomkejeli Raisi Wa Burundi Kupitia Michoro Wafurushwa Shuleni
    EAST AFRICA

    Wasichana Waliomkejeli Raisi Wa Burundi Kupitia Michoro Wafurushwa Shuleni

    Wycliffe NyamasegeBy Wycliffe NyamasegeApril 17, 2019No Comments2 Mins Read
    Share Facebook Twitter WhatsApp Telegram
    Picha ya Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza iliyofanywa kejeli na wasichana hao. [PICHA/ KWA HISANI]
    Share
    Facebook Twitter Telegram WhatsApp

    Wanafunzi watatu waliotiwa mbaroni mwezi uliopita kwa tuhuma za kumkejeli raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza wamefushwa shuleni siku chache baada ya kuachiliwa huru.

    Wasichana hao, na wengine wanne ambao waliachiliwa kwa njia tatanishi, walikamatwa kwa madai ya kumkejili raisi Nkurunziza kupitia michoro katika madaftari yao.

    Kukamatwa kwa wanafunzi hao kulikashifiwa katika mitandao ya kijamii haswa Twitter kwa kutumia hashitegi #FreeOurGirls.

    Wengi wanaamini kuwa mchango wao ndio uliopelekea wasichana hao wenye umri mdogo kuachiliwa.

    Duru za kuaminika zinaarifu kuwa licha ya kuachiliwa mwezi uliopita kutoka gereza la Ngozi walimokuwa wamefungiwa, serikali haikutupilia mbali kesi dhidi yao.

    Kulingana na shirika la kupigania haki za kibinadamu almaarufu Human Rights Watch, kesi iyo ilichangia kufurushwa kwa wasichana hao shuleni.

    “Ni vizuri waliachiliwa lakini tumekuja kugundua kuwa serikali haikutupilia mbali kesi dhidi yao, watatu hao sasa wamefurushwa shuleni, ” mkurugenzi wa shirika la HRW alidokezea vyombo vya habari.

    Mudge alidokeza kuwa wanafunzi hao, waliokuwa wakisomea shule ya Ecofo Akamuri iliyoko Kirundo, nchini Burundi, hawana budi ila kusalia nyumbani.

    Kulingana na barua kutoka shule iyo iliyoandikwa Machi 20, wanafunzi hao walienda kinyume na sheria za masomo katika kituo hicho cha mafundisho.

    “Kwa mjibu wa sheria za shule hii, kipengele cha 31 aya ya 28, wanafunzi hawa watano wamefurushwa kutoka shule hii,” barua iyo ambayo imetiwa sahihi na mkuu wa shule iyo Isaie Nkinzingabo imenukuliwa.

    Soma:Burundi Yawaachilia Huru Wanafunzi Waliomkejeli Raisi Nkurunziza Kupitia Michoro

    Nkinzingabo aliwaagiza wanafunzi hao kutafuta shule nyingine ili kuyaendeleza masomo yao.

    Kulingana na HRW, si mara ya kwanza visa kama ivyo kushuhudiwa nchini Burundi.

    Mwaka wa 2016, wanafunzi wanane wa shule ya upili walikamatwa kwa madai ya kumshurutisha raisi Nkurunziza atoke mamlakani kupitia kwa madaftari yao.

    Mwaka huo huo, mamia ya wanafunzi walikamatwa kwa tuhuma za kumkashfu Rais baada ya kuchora michoro isiyofaa dhidi yake.

    Watetezi wa haki za kibinadamu nchini humo wamekashifu utawala wa Rais Nkurunziza kwa wanachokitaja kuwa unyanyasaji wa haki za wanafunzi wasiokubaliana na uongozi wake.

    Raisi Nkurunziza aliingia mamlakani mnamo mwaka 2005. Aliweza kuchaguliwa tena mwaka wa 2015 licha ya upinzani mkubwa kutoka kwa wananchi kwa madai ya kuzidisha kipindi chake ofisini.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874

    Burundi Pierre Nkurunziza
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter) Follow on Instagram
    Share. Facebook Twitter Email Telegram WhatsApp
    Wycliffe Nyamasege

    Email news@localhost

    Related Posts

    Uproar as Matatu Linked to Ruto’s Son Flouts Rules as Police Watch

    January 9, 2025

    Morara Kebaso Responds To KRA Probe On Taxes, Terms It Political Witch-Hunt

    January 9, 2025

    Ugandan Nanny in Robbery Drama in Eastleigh Charged in Court

    January 9, 2025

    Nairobi County Govt Imposes New Restrictions On Hawkers In CBD

    January 9, 2025
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.







    Latest Posts
    SPORTS

    Everton sack manager Dyche with club 16th in Premier League

    By Oki Bin OkiJanuary 10, 2025

    Sean Dyche has been sacked as Everton manager after less than two years in charge…

    WORLD NEWS

    Swiss citizen dies in Iran prison after spying arrest

    By Oki Bin OkiJanuary 10, 2025

    A Swiss national arrested in Iran and accused of spying has died in prison, according…

    WORLD NEWS

    Jimmy Carter unites US as presidents attend state funeral

    By Oki Bin OkiJanuary 10, 2025

    Jimmy Carter brought a brief moment of national unity to a divided America Thursday as…

    WORLD NEWS

    Army Chief Joseph Aoun Elected Lebanon’s President After Years of Deadlock

    By KahawaTungu ReporterJanuary 9, 2025

    Lebanon’s parliament has elected the country’s army chief as president, ending a power vacuum that…

    KNOW YOUR CELEBRITY

    Colin Cowherd Siblings: All About Marlene

    By Kevin KoechJanuary 9, 2025

    Colin Cowherd is a prominent American sports media personality, best known for hosting The Herd…

    KahawaTungu
    Facebook X (Twitter) Instagram YouTube WhatsApp Telegram
    • Advertise
    • Disclaimer
    • Terms & Conditions
    • Contact Us
    © 2025 Kahawatungu.com

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.

    Go to mobile version